Drogba ajiunga na Shanghai ya Uchina.


Didier Drogba na Jose Mourinho

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Chelsea Didier Drogba anatarajiwa kujiunga na klabu ya Uchina ya Shanghai Shenhua wiki hii.

Mchezaji huyo anayetokea Ivory Coast mwenye umri wa miaka 34 amesema akubali kujiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili na nusu kwa mkataba upatao takribani paundi mill 25.

Drogba atatangaza kuhusu kujiunga na klabu hiyo rasmi kupitia mtandao wake mwenyewe (website) alisema kiongozi wa Shanghai.

Timu ya Al Wasl ya Uarabuni ilikuwa nayo yamtaka mchezaji huyo lakini Shanghai ndio imeshinda mbio hizo za kumnyakuwa Drogba.

“Hatua ya maisha yangu inayofuatia ni ya kufurahisha, ila ntatangaza mambo yote katika mtandao wangu hivi karibuni” alisema Drogba.

Chanzo: Dailymail

Posted on June 19, 2012, in Mpira, Mpira kwa Dakika, Tetesi and tagged , , . Bookmark the permalink. Leave a comment.

Comment